Jeremiah 12:1-3

Lalamiko La Yeremia


1 aWewe daima u mwenye haki, Ee Bwana,
niletapo mashtaka mbele yako.
Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako:
Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa?
Kwa nini wasio waaminifu
wote wanaishi kwa raha?

2 bUmewapanda, nao wameota,
wanakua na kuzaa matunda.
Daima u midomoni mwao,
lakini mbali na mioyo yao.

3 cHata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana;
unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe.
Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa!
Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
Copyright information for SwhKC